SIMBA YAING’ARISHA TANZANIA KWA USHINDI CAF, RAIS SAMIA ATOA PONGEZI
Wachezaji wa Simba walicheza kwa nidhamu ya hali ya juu na umoja mkubwa, wakihakikisha wanapata matokeo mazuri nyumbani. Ushindi huo umeifanya Simba kufuzu hatua ya Nusu Fainali ya michuano hiyo ya kimataifa, hatua inayodhihirisha ukuaji na ushindani wa soka la Tanzania katika ngazi ya Afrika.
PONGEZI KUTOKA KWA RAIS SAMIA
Baada ya ushindi huo wa kishujaa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kupitia akaunti yake rasmi ya WhatsApp siku ya Jumatano, aliandika:
> “Pongezi za dhati kwa Klabu ya Simba kwa ushindi katika mchezo wa mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup). Ushindi wenu ni furaha kwa mashabiki wenu na burudani kwa Watanzania wote. Ninawatakia kila la kheri katika Nusu Fainali.”
Kauli hiyo ya Rais imepokewa kwa shangwe na mashabiki wa Simba na Watanzania kwa ujumla, ikiwa ni ishara ya namna ambavyo michezo inavyounganisha taifa na kuleta mshikamano.
SIMBA: TUNAENDA KULETA TAJI NYUMBANI
Uongozi wa Simba umemshukuru Rais Samia kwa pongezi zake, na kuahidi kupambana kwa nguvu zaidi katika hatua ya Nusu Fainali. Mashabiki wa timu hiyo nao wameendelea kutoa sapoti kubwa, wakiamini kuwa mwaka huu ni fursa ya kihistoria kwa Simba kutwaa taji hilo kubwa la Afrika.
USISAHAU SUBSCRIBE YOUTUBE CHANNEL YETU | MY MEDIA DIGITAL. GUSA HAPA 👇




