ZANZIBAR KUJENGEWA UWEZO WA KITAALUMA NA KITEKNOLOJIA
Rais Dkt. Mwinyi ameshuhudia utiaji saini wa mikataba muhimu kati ya taasisi za Zanzibar na mashirika ya kimataifa, jambo linaloashiria juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kiteknolojia
Kuimarishwa kwa Sekta ya Uchumi wa Buluu na Uwekezaji:
Makubaliano hayo yanalenga kukuza uchumi wa buluu kupitia ushirikiano na taasisi kama Nutri-San Limited, SAMS (Scottish Association for Marine Science) na Royal Agriculture University, hivyo kusaidia matumizi bora ya rasilimali za baharini na kuongeza ajira kwa vijana.
Ushirikiano na taasisi kama Geopartners Ltd na vyuo vikuu vya Uingereza utasaidia Zanzibar kupata maarifa ya kisasa katika utafiti wa mafuta na gesi, pamoja na teknolojia ya kisasa ya kilimo na bahari.